Tuesday, 14 April 2015

ETOILE YAIVUTIA PUMZI YANGA..

Klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia inatarajiwa kuwasili Dar es Salaam wiki hii kwa ajili ya mechi yao ya kukata na shoka dhidi ya Yanga katika kombe la vilabu la Shirikisho barani Afrika.
Habari kutoka Yanga zinasema wapinzani wao wanaweza kutinga Dar es Salaam kati ya Alhamisi au Ijumaa kwa mechi ya kwanza itakayochezwa kati ya April 17 au 18 uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Mechi ya marudiano itachezwa Tunis, Tunisia baada ya wiki mbili.
Yaanza imeanza kuwavutia kasi wapinzani wao kufuatia wimbi la ushindi katika mechi zake za Ligi kuu.
Katika mechi za hivi karibuni, mabingwa hao wa zamani waliweka historia ya mvua ya magoli katika msimu baada kwa kuipa Coastal Union kichapo cha 8-0 na baadae Mbeya City 3-1 na kujikita kileleni ikiwa name pointi 46.
Tayari kocha wa Yanga, Hans Pluijm amewaonya wachezaji wake kuwa makini na kuweka akilini kuwa watakutana na moja ya timu ngumu barani Afrika katika hatua ya 16 bora .
Yanga iliwatoa Wazimbabwe, Platinum FC na sasa itatumia mechi zake za ligi kuu kama sehemu ya mazoezi kwa ajili ya mechi hiyo muhimu.

MASKINI.....WEMA,AZOMEWA LICHA YA KUJIELEZA.

Muigizaji maarafu wa filamu nchini Tanzania,Wema Sepetu alizomewa kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram
baada ya kuweka picha ya mlimbwende Hamisa Obetto akiwa mjamzito na kuandika maneno ya mshangao
”Jamani my mdogo umezaa.!wewe ni mwanamke sasa”.
Ujumbe huo ulizusha tafrani kwa baadhi ya watu na kumjibu Wema kwa maneno makali yenye kebehi ya
kwa nini yeye hazai anakaa kushabikia watoto wa wenzie tu.
Gumzo hilo lilifwata mkondo tofauti pale ambapo mchumba wake wa zamani mwanamuziki Diamond Platinum
akitarajia kupata mtoto na bi.Zari kutoka Uganda ambaye ni mpinzani wake mkubwa Wema.
Wema Sepetu aliweza kujibu tuhuma hizo kwa kusema yeye si mpanga wa yote,''ningekuwa na uwezo wa kuzaa angezaa siku nyingi ila ni Mungu ndiye anapanga'',
Alisema kuwa ''nimekuwa nikihangaika kupata mtoto usiku na mchana''
aliongezea kusema kuwa si rahisi kwa yeye kuwaambia kila kitu,kwani yeye pia ni binadamu na kuwa
''anaumia sana na maneno makali watu wanayoandika au kusema kumhusu''.
Ujumbe wa simanzi kutoka kwa muigizaji huyo ulirudiwa na baadhi ya waigizaji kama Iren Uwoya na mashabiki wengine
ukionya tabia ya watu kutoa matusi makali kwa Wema bila kuangalia upande wa pili,maana siku hizi kuna team kwenye mtandao pia zikijiita team Wema na Team Zari

Wednesday, 8 April 2015

HII SASA NI SIFA...YANGA YAIFUMUA COASTAL 8

Yanga hii ni ya kimataifa na kitaifa ndiyo habari ya mjini Coastal Union hawatasahau milele kipigo cha jana tarehe 8 mwezi wa 4 wapigwa bao sawa na tarehe ya siku ya mchezo wao na Yanga taifa. Amis Tambwe apiga nne, Mliberia  nae afunga bao lake la kwanza toka ajiunge Yanga na baada ya kufunga bao hilo alitoa machozi kwa furaha pia mliberia huyo alitoa pasi tatu zilizo zaa mabao matatu katika mchezo huo. Yanga sasa inazidi kujikita kileleni kwa kuwa na point 43 wakishuka dimbani mara 20, Azam baada ya kukabwa koo leo na Mbeya City kwa kufungana bao 1 kwa 1 wamebakia na point 37 baada ya kushuka dimbani mara 19. Wafungaji wa mabao  Tambwe nne, Msuva mbili Mliberia moja na Telela moja.
Hadi mwisho wa mchezo Yanga 8 na Coastal Union 0.