Wednesday, 8 April 2015

HII SASA NI SIFA...YANGA YAIFUMUA COASTAL 8

Yanga hii ni ya kimataifa na kitaifa ndiyo habari ya mjini Coastal Union hawatasahau milele kipigo cha jana tarehe 8 mwezi wa 4 wapigwa bao sawa na tarehe ya siku ya mchezo wao na Yanga taifa. Amis Tambwe apiga nne, Mliberia  nae afunga bao lake la kwanza toka ajiunge Yanga na baada ya kufunga bao hilo alitoa machozi kwa furaha pia mliberia huyo alitoa pasi tatu zilizo zaa mabao matatu katika mchezo huo. Yanga sasa inazidi kujikita kileleni kwa kuwa na point 43 wakishuka dimbani mara 20, Azam baada ya kukabwa koo leo na Mbeya City kwa kufungana bao 1 kwa 1 wamebakia na point 37 baada ya kushuka dimbani mara 19. Wafungaji wa mabao  Tambwe nne, Msuva mbili Mliberia moja na Telela moja.
Hadi mwisho wa mchezo Yanga 8 na Coastal Union 0.

No comments:

Post a Comment